Katibu wa Masuala ya EAC, Caroline Karugu, amesema, ushirikiano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unapaswa kusonga mbele zaidi ya ushirikiano wa kidiplomasia hadi kuunda ajira, kuongeza uzalishaji na kuimarisha usalama wa kikanda. Alibaini kuwa mafanikio ya ushirikiano wa kikanda yatapimwa kwa jinsi unavyoboresha maisha kupitia biashara iliyopanuliwa, kusafiri kwa watu na bidhaa kusiko na vikwazo, na ushirikiano imara zaidi. Karugu alisisitiza kwamba sera za biashara zilizoratibiwa, mifumo bora ya forodha na miundombinu bora ya usafiri ni muhimu katika kufungua uwezo wa kiuchumi wa kanda.