Rais William Ruto amehimiza kuanzishwa kwa mkataba mpya wa kitaifa wa muda mrefu ili kuelekeza mabadiliko ya kiuchumi ya Kenya zaidi ya Dira ya mwaka 2030. Katika hotuba ya kitaifa, alisema ajenda inayofuata ya maendeleo lazima ipite siasa na mizunguko ya uchaguzi. Rais alitaka mazungumzo mapana na jumuishi kuhusu mustakabali wa nchi, akisisitiza kwamba mfumo huo unapaswa kukitishwa kwenye katika Katiba ya 2010 na kuendana na matarajio ya muda mrefu ya Kenya ya ukuaji endelevu na jumuishi.


WILLIAM RUTO - DECISIONS