Naibu Kiongozi wa Chama cha Jubilee Fred Matiang'i amepuuza pendekezo la Rais William Ruto la mazungumzo ya kitaifa kuhusu maendeleo ya Kenya zaidi ya ruwaza ya 2030, akiitaja kuwa kipaumbele kisichofaa. Matiang'i anasema nchi inapaswa kwanza kushughulikia kile anachokielezea kama ukiukaji wa kikatiba, ukosefu wa usalama na kudhoofika kwa taasisi za umma. Pia aliishutumu serikali kwa kushindwa kutimiza ahadi za zamani, akisema Wakenya wanastahili uongozi unaowajibika kabla ya Uchaguzi Mkuu wa 2027.