Jaji Mkuu wa zamani David Maraga amekosoa hotuba ya kitaifa ya Rais William Ruto, akihoji kama faida za kiuchumi za serikali zimeboresha maisha ya Wakenya wa kawaida. Maraga, ambaye anawania urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2027 aliwaomba Wakenya kutathmini hali yao ya kiuchumi tangu Ruto alipoingia madarakani, akizungumzia gharama ya chakula, mafuta na elimu.