Vikundi vya ushawishi vimewasilisha ombi kwa Bunge la Kitaifa kusimamisha mikopo ya umma kwa miaka miwili kuanzia mwaka wa fedha wa 2027/28, wakisema deni linaloongezeka la Kenya limekuwa lisiloweza kuthbitika. Bunge Mashinani na Mtandao wa Uwezeshaji wa Kaunti ya Kiambu wanasema deni la umma limeongezeka kutoka takriban Sh trilioni 2.4 mwaka wa 2014 hadi zaidi ya Sh trilioni 12, huku malipo ya deni yakichukua sehemu kubwa ya mapato ya kodi. Wanataka nidhamu kali ya fedha, usimamizi imara wa bunge na marekebisho ya Sheria ya Usimamizi wa Fedha za Umma ili kupunguza ukopaji kupita kiasi.