Jaji Mkuu Martha Koome ametoa wito wa kupitishwa kwa haraka kwa Muswada wa Makosa ya Kijinsia, akisema sheria kali zinahitajika ili kukabiliana na visa vinavyoongezeka vya unyanyasaji wa kingono na kijinsia nchini. Koome alisema kukomesha uovu huo kutahitaji mageuzi ya kisheria, kitaasisi, na sera yaliyoratibiwa. Zaidi ya hayo, ametoa wito wa adhabu kali kwa wahalifu na kuanzishwa kwa kitengo maalum cha usalama ili kusaidia kukabiliana na visa vinavyoongezeka vya mauaji ya wanawake.

MARTHA KOOME-STIFF