Harambee Starlets walipokea kichapo cha mabao 4-0 kutoka kwa wenyeji Morocco katika mechi yao yao ya kwanza ya WAFCON katika Uwanja wa El Hassan huko Rabat jana usiku. Sakina Ouzraoui alifungua ukurasa wa mabao dakika ya 19 kabla ya Maryame Atiq kuongeza bao la pili dakika tisa baadaye. Ibtissam Jraïdi aliongeza bao la tatu la Morocco dakika ya 32, kabla ya kukamilisha mabao yake mawili dakika ya 47. Ushindi huo uliifanya Morocco kupanda kileleni mwa kundi A, ikiwa na pointi tatu sawa na Algeria iliyoshinda Senegal 2-0, lakini ikiwa na tofauti ya mabao.


PSG wamejiondoa kwenye mbio za kumsajili mshambuliaji wa RB Leipzig Yan Diomande, huku Real Madrid sasa ikiwa na uhakika wa kumpata mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast. Madrid, ambayo tayari imekataliwa ofa ya zaidi ya pauni milioni 85 kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 19, huku Leipzig ikitaka pesa zaidi ili kumwachilia, inaeleweka kuwa inajitahidi sana kukamilisha dili kwa mchezaji huyo. Real pia wamekubaliana masharti binafsi na Diomande. Liverpool pia wameonyesha nia ya kumsajili Diomande, lakini hawako tayari kulipa zaidi ya pauni milioni 85.


Vipindi vya anga kavu vinashuhudiwa Nairobi.

Ili kupata habari zaidi tembelea tovuti ya radiojambo.