Naibu Rais wa zamani Rigathi Gachagua amemshutumu Waziri wa Usalama Kipchumba Murkomen kwa vitendo ambavyo anadai vimechangia ukosefu wa usalama nchini. Kiongozi huyo wa DCP alidai kwamba pasipoti za kidiplomasia zilitolewa kwa raia wa kigeni na kwamba vitambulisho vya kitaifa vilikuwa vikitolewa kinyume cha sheria kwa wageni. Alidai zaidi kwamba vitendo hivyo vinavyodaiwa vinahatarisha amani ya kikanda. Waziri Murkomen anatarajiwa kujibu madai hayo.
RIGATHI GACCHAGUA – MURKOMEN