Mwenyekiti wa Baraza la Magavana Ahmed Abdullahi ameishutumu Wizara ya Afya kwa kuchochea migomo ya mara kwa mara ya wafanyakazi wa afya kwa kushindwa kuheshimu makubaliano ya ufadhili na utawala, akisisitiza serikali za kaunti zinalaumiwa isivyo haki kwa kuvuruga huduma za afya za umma. Gavana huyo wa Wajir alisema wizara, pamoja na mashirika mengine ya serikali ya kitaifa, imeshindwa kutekeleza makubaliano muhimu ya serikali, na kusababisha migomo ya mara kwa mara ya madaktari na wafanyakazi wa UHC.
AHMED ABDULLAHI – STRIKES