Serikali inashirikiana na benki, taasisi za fedha za maendeleo na washirika wa kimataifa ili kuboresha upatikanaji wa mikopo nafuu kwa biashara ndogo. Katibu wa MSME Susan Mang'eni anasema jopokazi linalowaleta wakopeshaji kinapitia mifumo ya kugawana hatari ili kurahisisha upatikanaji wa fedha. Anasema ufadhili unaotabirika utawawezesha wajasiriamali kupanua biashara zao, kuunda ajira na kujenga biashara endelevu.

SUSAN MANG'ENI – MSMEs