Kenya inatafuta kuimarisha utafiti wa chanjo na utengenezaji wa humu nchini kupitia ushirikiano na Mpango wa Kimataifa wa Chanjo ya UKIMWI. Waziri wa Afya Aden Duale anasema ushirikiano huo utazingatia utafiti wa chanjo, majaribio ya kimatibabu, uhamishaji wa teknolojia na maendeleo ya nguvu kazi kwa Virusi vya HIV, Kifua Kikuu na magonjwa ya kuambukiza yanayoibuka. Anasema mpango huo pia utaunga mkono juhudi za Taasisi ya BioVax ya Kenya za kuongeza uzalishaji wa chanjo na bidhaa zingine za afya ya kibiolojia.