Rais wa FKF Hussein Mohammed na Mkurugenzi Mtendaji Dennis Gicheru wanatarajiwa kukutana na vilabu vya KPL asubuhi ya leo ili kuepuka mgogoro unaonukia kabla ya msimu wa 2026/27. Mkutano huo unakuja baada ya vilabu kusisitiza kwamba havitaanza kampeni mpya bila utekelezaji wa Kamati ya Mpito iliyokubaliwa kusimamia ligi. Vilabu hivyo vilikuwa vimealika Kamati nzima ya Utendaji ya Kitaifa ya FKF kwa mazungumzo Jumanne, lakini Mkurugenzi Mtendaji wa FKF Gicheru aliwafahamisha kwamba Rais Mohammed alikuwa nje ya nchi na hayupo kwa mkutano huo.

Tusker FC inatarajiwa kukamilisha usajili wa kipa wa kimataifa wa Congo Perrauld Ndinga kabla ya msimu wa 2026/27, huku mkataba huo ukiwa katika hatua zake za mwisho. Hii inafuatia kuondoka kwa kipa mwenzake wa Congo Pavelh Ndzila kwenda Shabana FC, baada ya mkataba wake wa muda mfupi kuisha mwezi uliopita. Ndzila alijiunga na brewers Januari kutoka kwa mabingwa wa Rwanda Rayon Sports. Aliendelea kuwa kipa chaguo la kwanza na kuwasaidia kushinda kombe la FKF msimu uliopita na kufuzu kwa kombe la mashirikisho la CAF.

Vipindi vya anga kavu vinashuhudiwa Kakamega, Eldoret na Kisumu.

Ili kupata habari zaidi tembelea tovuti ya radiojambo.