Naibu Rais Kithure Kindiki anasema serikali haitavumilia maandamano ya vurugu yanayojificha kama utekelezaji wa haki za kikatiba. Akizungumza huko Machakos, Kindiki alisema ingawa uhuru wa kujieleza unalindwa na sheria, haupaswi kutumika kuchochea vurugu, kuharibu mali au kudhoofisha utulivu wa umma. Alionya kwamba wale wanaohusika katika vitendo vya uhalifu wakati wa maandamano watakabiliwa na nguvu kamili ya sheria.
KITHURE KIDNIKI – VIOLENCE