Nahodha msaidizi wa zamani wa AFC Leopards, Ken Owino, yuko karibu kujiunga na Ulinzi Stars, baada ya kuondoka Ingwe mwezi uliopita baada ya mkataba wake kuisha. Alijiunga na mwenzake wa zamani Shawn Oloo na mshambuliaji wa Tusker FC, Jacob Onyango, ambao pia wametia saini mkataba na KDF. Kwingineko mshambuliaji wa Gambia, Musa Ceesay, amejiunga na Ingwe, huku mlinzi Lameck Omondi akipatikana kama mchezaji huru baada ya kuondoka Mara Sugar baada ya mkataba wake kuisha.
Timu ya Kenya kwenye Michezo ya Jumuiya ya Madola ya Glasgow ya mwaka 2026 imepigwa jeki kifedha baada ya serikali kuboresha mpango wa zawadi kwa walioshinda medali. Kulingana na Katibu wa Michezo, Elijah Mwangi, walioshinda medali za dhahabu watapokea ksh milioni 2.5 kwa kila medali, huku walioshinda medali za fedha wakipata Ksh milioni 1.5 na washindi wa shaba wakipata Ksh milioni 1. Bingwa wa zamani wa dunia wa kurusha mkuki, Julius Yego, atakuwa nahodha wa timu hiyo ya wanariadha 94 waliochaguliwa kutoka taaluma 12 za michezo. Kenya ilishinda jumla ya medali 21 mwaka wa 2022 na itataka kuboresha idadi hiyo.
Vipindi vya anga kavu vinashuhudiwa Nairobi, Narok na Kajiado.
Ili kupata habari zaidi tembelea tovuti ya radiojambo.