Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna anataka Kamati ya Elimu ya Seneti iingilie kati kuhusu mpango wa Shahada ya Sanaa katika Ukarimu iliyokwama katika Chuo Kikuu cha Nairobi. Sifuna anasema kozi hiyo imeendelea kusimamishwa tangu mwaka 2024 baada ya makubaliano ya ushirikiano kati ya chuo hicho na Chuo cha Kenya Utalii kuisha, na kuwaacha wanafunzi waliojiandikisha katika hali ya kutokuwa na uhakika.
EDWIN SIFUNA – STUDENTS