Naibu Rais Kithure Kindiki anasema mpango wa NYOTA utawasaidia vijana kupata ujuzi walioupata nje ya elimu rasmi kupitia mpango wa Kutambua Masomo ya Awali. Akizungumza huko Nakuru, Kindiki alisema mpango huo utawapa vijana ithibati kulingana na ujuzi wao uliopo, na kuwawezesha kupata fursa za ajira nchini Kenya na nje ya nchi. Alisema ithibati hiyo itasaidia kuziba pengo kati ya ujuzi usio rasmi na soko la ajira.
KITHURE KINDIKI – EMPOWERS