Mtoto aliyezaliwa kutokana na upandikizaji wa tumbo la uzazi//HISANI

TAIFA la Uingereza limetangaza kisa chake cha kwanza cha ufanisi wa kisayansi ambapo mwanamke aliyepandikiziwa tumbo la uzazi amejifungua mtoto wa kike salama salimini.

Kwa mujibu wa The Guardian, Mama wa mtoto huyo, Grace Davidson, 36, alizaliwa bila uterasi inayofanya kazi, na alipandikiziwa tumbo la dadake mnamo 2023 - katika kile ambacho wakati huo kilikuwa upandikizaji pekee wa Uingereza uliofanikiwa.

Miaka miwili baada ya mchakato huo wa upainia, Grace alijifungua mtoto wake wa kwanza mwezi wa Februari.

Yeye na mumewe, Angus, 37, wamempa binti yao Amy jina la dada wa Grace, ambaye alitoa tumbo lake.

Akiwa amempakata mtoto Amy - ambaye alikuwa na uzani wa zaidi ya kilo mbili (pauni nne na nusu) - kwa mara ya kwanza ilikuwa "ajabu" na "muujiza wa kweli", mama mpya Grace anasema.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

"Ilikuwa ngumu sana kwa sababu hatukuwahi kujiruhusu kufikiria jinsi ingekuwa kwake kuwa hapa," anasema. "Ilikuwa nzuri sana."

Grace na Angus, ambao wanaishi kaskazini mwa London lakini wanatoka Scotland, wanatumai kupata mtoto wa pili kwa kutumia tumbo la uzazi lililopandikizwa.

Awali wanandoa hao walitaka kuhifadhiwa majina yao, lakini kufuatia kuwasili salama kwa mtoto Amy sasa wanazungumza na BBC kuhusu "muujiza wao mdogo".

Timu ya upasuaji iliiambia BBC kuwa wamefanya upandikizaji mwingine watatu wa uzazi kwa kutumia wafadhili waliofariki tangu kupandikizwa kwa Grace. Wanalenga kutekeleza jumla ya 15 kama sehemu ya majaribio ya kimatibabu.

Mtoto wa kwanza aliyezaliwa kutokana na upandikizaji wa tumbo la uzazi alikuwa nchini Uswidi mwaka 2014.

Tangu wakati huo takriban upandikizaji 135 wa aina hiyo umefanywa katika zaidi ya nchi kumi na mbili, zikiwemo Marekani, China, Ufaransa, Ujerumani, India na Uturuki.

Takriban watoto 65 wamezaliwa.

Mtoto Amy alizaliwa kwa upasuaji katika hospitali ya Malkia Charlotte magharibi mwa London mnamo tarehe 27 Februari.

"Ilikuwa wakati mzuri sana, uliojaa furaha," anasema daktari wa upasuaji Isabel Quiroga.

Grace na Angus wanasema wanatumai kupata mtoto wa pili - punde tu timu ya madaktari itasema kuwa wakati umefika.