Mwalimu katika Kaunti ya Nyamira anauguza majeraha katika hospitali ya Ikonge baada ya kushambuliwa na mkuu wa shule  kwa madai ya kuchelewa.

Vincent Onyancha alisema alipigwa kofi na teke mbele ya wanafunzi wake.

 “Nilichelewa kidogo kufika shuleni na mkuu wa shule aliingia darasani na kunipiga nikiwa nafundisha," alisema.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Wakiwahutubia wanahabari mjini Ikonge, maafisa kutoka Chama cha Walimu wa Elimu ya Baada ya Msingi nchini Kenya (KUPPET) walilaani kisa hicho na kuitaka Tume ya Huduma kwa Walimu (TSC) kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mkuu wa shule, na kuongeza kuwa walimu wangesusia kufanya kazi kwa maandamano ikiwa hakuna hatua zinazochukuliwa.

Mkurugenzi wa TSC katika Kaunti ya Nyamira, Erick Magak, alithibitisha kupokea kesi hiyo, na  akasema  uchunguzi umeanzishwa.