
MWANAHARAKATI Morara Kebaso amekuwa mtu wa hivi punde
kutangaza rasmi azma yake kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao, 2027.
Kupitia ukurasa wake wa X, Kebaso aliandika sentensi
mbili tu za kuwahakikishia wafuasi wake utayarifu wake katika kinyang’anyiro
cha kuingia katika ikulu ya Nairobi.
Kiongozi huyo wa chama kipya kabisa humu nchini cha
INJECT alisema kwamba ana Imani ataibuka mshindi dhidi ya washindani wake,
akiwemo rais Ruto.
Kebaso alisema yeye atasimama akiwa na Imani kuu
katika kabila lake ambalo alilitaja kuwa ni vijana wa kizazi cha Gen Z.
“Nitawania
urais wa Kenya. Kabila langu litakuwa ni vijana wa Kenya,”
Kebaso alitangaza.
Tangazo lake lilijiri saa chache baada ya uvumi
kuibuliwa na gazeti moja la humu nchini kuhusu aliyekuwa waziri wa masuala ya
ndani Dkt Fred Matinag’i kulenga wadhifa wa urais pia.
Kebaso alionekana kutofautiana na Matinag’i
akimtuhumu kuwa aliyekuwa bosi wake, rais mstaaafu Uhuru Kenyatta alihusika
katika ufisadi, hivyo pia yeye [Matinag’i] hafai kuaminiwa na uongozi wa nchi.
“Bosi
na mfadhili wa Matiang’I, Uhuru Kenyatta alirithi deni la trilioni 1.89 kutoka
kwa Kibaki. Katika miaka kumi alikopa hadi trilioni 8.9. 80% ya pesa hizo
ziliibiwa,” Kebaso alisema.
Akionyesha matumaini ya kuwa rais wa 6 wa Kenya,
Kebaso alisema kwamba jambo la kwanza atakalolifanya ni kurudisha pesa za Kenya
zilizoibwa na wanasiasa na kufichwa nje ya nchi.
“Mojawapo
ya hatua zangu za kwanza kama Amiri Jeshi Mkuu itakuwa kurudisha pesa hizo
kutoka popote pale Pandora, Visiwa vya Cayman, Jiji la Jersey, London, Hong
Kong na hata hapa Kenya. Na simdanganyi na sifichi azma yangu. Ruto ni fisadi
tutamjia. Lakini pia tutatafuta bilioni 12 ambazo ziliibiwa kutoka kwa hazina
siku ya uchaguzi mnamo 2022,” alisema.
Alisema kwamba kuwafuata watu anaohisi ni wafisadi
hakutamsaza Matiang’i – jamaa anayedaiwa kuwa mshindani mwenzake, akisema kuwa
gavana wa Nyamira ni mradi wake.
“Pia tutaenda kwa mradi wa Matiang’i, Amos Nyaribo
gavana wa Kaunti ya Nyamira. Chapisha tweet hii. Nikiweka biblia chini
ichapishe kwenye gazeti,’ Kebaso alisema.
Wengine ambao tayari wameonyesha nia ya kuwania urais
ni pamoja na Kalonzo Musyoka wa Wiper, na Eugene Wamalwa wa DAP-K.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!