Kisa cha mwanamke aliyeripotiwa kutoweka kwa njia tatanishi kiligeuka na kuwa kama filamu ya kuchekesha baada ya mwanamke huyo kupatikana salama salimini nyumbani kwa mumewe.

Mwanamke huyo aliripotiwa kupotea na mpenzi wake ambaye alipiga ripoti polisi kuhusu kutoweka kwake.

Baada ya msako dhidi yake kuanzishwa, alipatikana akiwa ametulia kwa mumewe, jambo ambalo limekuwa mjadala pevu katika mitandao ya kijamii.

Ilivyobainika, mrembo huyo aliandaa kutekwa nyara kwake mwenyewe kwa usaidizi wa mumewe kwa nia ya kumuibia mpenzi wake pesa.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Huduma ya Kitaifa ya Polisi (NPS) ilitoa taarifa kamili jioni ya Jumamosi, Novemba 16, ikisimulia jinsi mshukiwa alipanga njama na mumewe kughushi utekaji nyara.

Mpenzi mwingine wa mwanamke huyo aliwasilisha ripoti akidai watekaji nyara walidai fidia ya Ksh150,000.

Kesi hiyo tangu wakati huo imekuwa ikivutia watu kote nchini huku Idara ya Uchunguzi wa Uhalifu (DCI) na Idara ya Ujasusi (CRIB) ikianzisha operesheni ya kumpata mwathiriwa nyara.

Uchunguzi zaidi ulipelekea wapelelezi hadi Narok Kusini, ambapo walimpata mwathiriwa katika nyumba ya mumewe. Wawili hao tangu wakati huo wametiwa mbaroni na polisi.

"Mnamo Novemba 16, 2024, timu hiyo ilielekea Oldonyo Orok, Narok Kusini ambako nambari ya mwathiriwa ilipatikana mwishowe, na kumpata nyumbani kwa mumewe," taarifa ya Huduma ya Kitaifa ya Polisi ilisoma.

Wawili hao tangu wakati huo wamesindikizwa hadi Nairobi, ambapo wanaweza kukabiliwa na mashtaka mazito yanayohusiana na kutoa taarifa za uongo kwa vyombo vya sheria, kosa chini ya Kifungu cha 129 cha Kanuni ya Adhabu.

Mapema mwezi wa Novemba, hadithi ya kutoweka kwa mwanamke huyo ilienea mitandaoni baada ya mumewe kwenda kwenye runinga kutoa maelezo ya kuhuzunisha lakini ya kutia shaka jinsi mkewe alishawishiwa na simu moja.