Mwanaharakati na mwanasiasa Morara Kebaso ameweka
wazi kwamba hatojiunga na chama au muungano wowote wa kisiasa humu nchini.
Mwanzilishi huyo wa chama cha INJECT aliwahakikishia
wafuasi wake kwenye ukurasa wake wa jukwaa la X kwamba hatoyumbishwa na
vuguvugu linaloendelea la kuwachukua vijana wote wa Gen Z katika vyama vikuu
vya kisiasa nchini.
“Kuna
jitihada kubwa sana za kuwameza viongozi wote wa GenZ kwenye vyama vya siasa
vya kawaida ili kuwafundisha mtindo wa kifisadi wa zamani. Ndio maana
tukaanzisha Chama cha INJECT. Tutapanga njia yetu wenyewe. Sitajiunga na UDA au
ODM au WIPER muda wao umekwisha. Ni wakati wetu sasa. Uthabiti hadi mwisho,”
Kebaso alisema.
Mwanaharakati huyo wa elimu ya kiraia katika sasisho
jingine, alifichua kwamba upo mpango wa kuingia katika ikulu japo hakusema ni
lini.
Kebaso aliwataka wanachama wake wote na vijana wote
kujiweka tayarikusafiri kuingia jijini Nairobi muda wowote, akidokeza kwamba
kutakuna na vuguvugu kuu la kuingia kaitka ikulu ya Nairobi.
Alisisitiza kwamba mchakato huo hautakuwa rahisi kwa
watu waoga, akisema kwamba kila kijana anastahili kufungia woga wake kwenye
sanduku kabla ya kusafiri kuja Nairobi.
“Anza
kujitayarisha. Tunaandamana hadi Ikulu hivi karibuni. Jitayarishe kusafiri
kutoka kila mahali nchini Kenya hadi Nairobi. Jitayarishe kupiga kambi mjini.
Tuna mgawo wa pekee unaohitaji watu wasio na woga. Chukua hofu yako na uifunge
kwenye sanduku na kufuli mbili. TUNAKUHITAJI USIOGOPE. Jitayarishe na usubiri
ishara,” Kebaso alisema.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!