Mvulana mmoja ambaye ni mtahiniwa a mtihani wa kitaifa wa KCSE mwaka huu katika kaunti ya Bomet ametiwa mbaroni baada ya kushukiwa kumlawiti mvulana wa miaka 7.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo ya kustaajabisha, mvulana huyo mwenye umri wa miaka 19 anadaiwa kumhandaa mvulana wa miaka 7 kwa peremende na soda kabla ya kumtendea unyama huo.

Citizen wanaripoti kwamba kamanda wa polisi wa kaunti ndogo ya Konoin, alithibitisha kisa hicho akisema mshukiwa aliripotiwa kutekeleza kitendo hicho kiovu kwa nyakati tofauti kabla ya kukamatwa.

"Ni tukio la kusikitisha na tunafanya kila linalowezekana ili kupata kiini cha suala hilo, haki za watoto zilindwe kwa gharama yoyote. Tunatoa wito kwa yeyote mwenye taarifa zaidi atusaidie katika uchunguzi," kamanda huyo wa polisi alinukuliwa.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Inaarifiwa kwamba hii si mara ya kwanza kwa mvulana huyo kufanya kitendo hicho cha ukatili kwa mtoto huyo, kila mara akimhadaa kwa pipi na soda.

Mshukiwa huyo atakuwa anafanya mtihani wake wa KCSE chini ya ulinzi mkali korokoroni.

Mitihani ya KCSE ilianza mapema wiki jana na tayari vvisa kadhaa vya utovu wa kimaadili vimeripotiwa kando na visa vya wizi wa mtihani huo.

Wikendi iliyopita, wavulana kadhaa wa shule ya sekondari ya Shiners jijini Nakuru walitiwa mbaroni baada ya kudaiwa kuhusika katika mauaji ya mtahiniwa mwenzao shuleni.

Kwa mujibu wa taarifa, wavulana hao mmoja wao alimchoma mwenzao kisu tumboni hadi kufa baada ya mfarakano wa kuibiwa baadhi ya vitu vyao kwenye bweni.