Chama cha Wamiliki wa Matatu kimewasihi NTSA na polisi kushirikiana na NICCO Sacco kumkamata dereva anayeshutumiwa kwa kumsukuma mwanafunzi wa KMTC kutoka kwenye gari linalosonga, badala ya kutoa zaidi ya magari 100 barabarani. Mwenyekiti Albert Karakacha anasema NICCO Sacco haina vifaa vya kutosha kumfuatilia dereva huyo, akionya kwamba kuondolewa kwa magari hayo pia kutasababisha hasara kubwa za biashara.
ALBERT KARAKACHA – ROGUE