Huku Kenya ikijiandaa kwa mvua kubwa inayoweza kutokea kuanzia Oktoba hadi Disemba, kumbukumbu za mafuriko mabaya yaliyokumba Nairobi mwezi Machi bado ni mpya kwa familia za Mathare. Miongoni mwa wale wanaoishi na makovu hayo ni Anne Wanjiku, ambaye alifiwa na mumewe baada ya kusombwa na maji alipokuwa akiwasaidia wakaazi kuvuka maji ya mafuriko. Sasa, huku msimu mwingine wa mvua ukikaribia, Wanjiku anataka serikali ichukue hatua kabla ya maji kufurika tena.
ANNE WANJIKU – FLOODS