Murang’a imeanzisha mpango wa chakula shuleni kote katika kaunti hiyo unaolenga zaidi ya wanafunzi elfu 215 katika shule za msingi za umma, JSS na vituo vya ECDE. Mpango huu unafuatia jaribio la miaka miwili lililofanikiwa lililofanywa katika shule 90 kote kaunti. Gavana Irungu Kang’ata alisema mpango huo utapanuliwa hadi shule zote za umma, huku serikali ya kaunti ikichukua hatua za kuhakikisha wanafunzi walio katika mazingira magumu wanahudumiwa huku ikiwasaidia wakulima wa eneo hilo.
IRUNGU KANG’AGTA – PROGRAM