Gavana wa Homa Bay Gladys Wanga amekaribisha mkutano wa hadhara wa Linda Mwananchi uliopangwa kufanyika katika kaunti hiyo, akisema vuguvugu hilo lina haki ya kikatiba ya kutembelea sehemu yoyote ya nchi. Wanga alipuuza madai kwamba viongozi wa eneo hilo walikuwa wameajiri wahuni kuvuruga mikutano hiyo, akiishutumu kundi la upinzani kwa kueneza propaganda ili kuongeza shauku katika mkutano huo. Alionya dhidi ya vurugu za kisiasa, machafuko na usumbufu wakati wa mkusanyiko uliyopangwa.
GLADYS WANGA - PEACE