Wabunge wameunga mkono Muswada unaotaka kuunda njia maalum kwa waendesha baiskeli na watembea kwa miguu kote nchini. Mswada wa Marekebisho ya Barabara za Kenya unaofadhiliwa na mbunge wa Samburu West Naisula Lesuuda, unawataka KeNHA, KeRRA na KURA kubuni na kujenga miundombinu ya usafiri isiyotumia injini, ikiwa ni pamoja na njia za baiskeli, njia za watembea kwa miguu na vivuko vya watembea kwa miguu. Mswada huo pia unawapa polisi mamlaka ya kushinikiza kutumiwa kwa vifaa hivyo maalum na kuwalinda waendesha baiskeli na watumiaji wengine wa usafiri usiotumia injini.