Serikali imezindua mpango wa ukuzaji ujuzi na riziki unaolenga vijana na wanawake 450 walio katika mazingira magumu katika kaunti za Nairobi, Kilifi, Kisumu, Isiolo na Samburu. Mpango huo, uliopewa jina la Maisha ya Ustahimilivu na Vijana Walio katika Mazingira Hatari, unalenga kushughulikia vichocheo vya kijamii na kiuchumi vya itikadi kali huku ukiimarisha ustahimilivu wa jamii. Katibu wa usalama Raymond Omollo alisema amani endelevu inahitaji kukabiliana na hali za kijamii na kiuchumi zinazoweka jamii zilizo katika mazingira magumu katika uhalifu, siasa kali na itikadi kali.
RAYMOND OMOLLO - DEAL