Wakenya bado wanasajiliwa kupigana katika vita vya Urusi na Ukraine licha ya makubaliano ya awali kati ya Kenya na Moscow ya kusitisha usajili huo, kulingana na tume ya haki za binadamu nchini. Mshauri wa KHRC Odhiambo Ojiro anasema baadhi ya Wakenya ambao wamerudi kutoka Urusi wanashawishiwa kurudi na kuendelea kupigana. Ojiro ameibua wasiwasi kuhusu kuendelea kuajiri, akitaka uchunguzi zaidi wa hali ambayo Wakenya wanasajiliwa katika jeshi la Urusi.


ODHIAMBO OJIRO – RECRUITMENT