Nairobi United imekamilisha ziara yao ya maandalizi ya msimu nchini Uganda kwa ushindi, baada ya kuishinda KCCA FC 2-1 katika mechi yao ya mwisho ya kirafiki. Michael Karamor alikuwa nyota wa mechi hiyo, akifunga mabao yote mawili na kuihakikishia ushindi timu hiyo ya Kenya. Timu hiyo inatarajiwa kurudi nchini, jioni hii kabla ya msimu mpya wa KPL. Mechi zingine za kirafiki za maandalizi ya msimu zilishuhudia, Mathare United ikifungwa 1-0 na APR ya Rwanda katika uwanja wa Dandora jana, huku AFC Leopards ikiwashinda wapinzani wao wa humu nchini Kakamega Homeboyz 2-0 katika uwanja wa Bukhungu.


Mwanariadha wa masafa ya kati kutoka Marekani mzaliwa wa Kenya, Jonah Koech, amepigwa marufuku kushiriki mchezo huo kwa miaka mitatu kwa kutumia dawa za kuongeza nguvu mwilini. Shirika la Kupambana na Dawa za kuongeza nguvu mwilini la Marekani linasema ukiukaji wa matumizi ya dawa hizo kwa Koech ulibainika kufuatia viwango vya juu kwenye damu katika uchunguzi wa kibayolojia. Koech alishinda kwa kushangaza katika mbio za mita 1500 za wanaume katika Mashindano ya Nje ya Marekani mwaka uliopita, akimaliza mbele ya Ethan Strand na mshindi wa medali ya dhahabu ya Olimpiki ya 2024, Cole Hocker, katika rekodi ya dakika 3 na sekunde 30. Cheo chake sasa kimeondolewa baada ya kukubali matumizi ya dawa iliyopigwa marufuku.



Vipindi vya anga kavu vinashuhudiwa Nairobi, Kajiado na Narok.

Ili kupata habari zaidi tembelea tovuti ya radiojambo.