Mteuliwa wa mwenyekiti wa IPOA Duncan Ojwang ameahidi "kusema ukweli kwa mamlaka" na kutetea haki za Wakenya ikiwa ataidhinishwa kuongoza chombo hicho cha usimamizi wa polisi. Akiwa mbele ya Kamati ya Usalama ya Bunge la Kitaifa kwa ajili ya kuchunguzwa, Ojwang aliapa kudumisha uhuru wa IPOA huku akishirikiana na Huduma ya Kitaifa ya Polisi ili kuboresha ulinzi na kurejesha imani ya umma. Alisema jukumu kuu la IPOA ni kuwalinda raia na kuhakikisha polisi wanatumia mamlaka yao ndani ya Katiba na sheria.
DUNCAN OJWANG - CAMERA