Waziri wa Nishati, Opiyo Wandayi, ametoa changamoto kwa taasisi zote kukumbatia nishati mbadala kama sehemu ya mpango mkubwa wa kupunguza gharama ya umeme nchini. Waziri huyo alisema hatua hiyo, mbali na kushughulikia athari mbaya za kukatika kwa umeme, pia itawezesha chanzo cha umeme rafiki kwa mazingira kuchochea ukuaji wa uchumi nchini. Wandayi alizungumza baada ya kuzindua Mfumo Mseto wa Nishati ya Jua katika Gereza la Usalama la Nairobi.OPIYO WANDAYI - INVESTMENTS