Donald Trump, Barrack Obama

RAIS wa Marekani, Donald Trump amedokeza kuwa yuko tayari kuwania urais kwa muhula mwingine – wa 3 – nhini humo kinyume na takwa la kikatiba kwa rais kuhudumu kwa mihula miwili pekee.

Akizungumza na mwanahabari wa NBC News, Trump alisema kuwa ni wanachama wa Republican ambao wamekuwa wakimshinikiza kuwania muhula mwingine tena katika uchaguzi wa 2028.

"Watu wengi wanataka niwanie," aliambia NBC News. "Lakini, ninamaanisha, kimsingi ninawaambia tuna safari ndefu, unajua, ni mapema sana katika utawala. Sifanyi mzaha," alisema.

Baada ya kudai hivyo, wanachama wa Democrats pia walishinikiza ikiwa atawania itabidi pia wamwasilishe rais wa zamani Barack Obama kuwania dhidi ya Trump.

"Najua ni dhahania hivi sasa, lakini ikiwa unaruhusiwa kwa sababu fulani kugombea muhula wa tatu, kuna wazo kwamba Wanademokrati wanaweza kujaribu kumwasilisha Barack Obama dhidi yako?" Mwandishi wa Fox News Peter Doocy alimuuliza Trump katika Ofisi ya Oval.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

"Ningependa hiyo. Hiyo itakuwa nzuri. Ningependa hiyo," Trump alijibu.

"Hapana, watu wananiuliza nigombee. Sijui, sikuwahi kuichunguza. Na wanasema kuna njia unaweza kufanya hivyo, lakini sijui kuhusu hilo," Trump aliendelea. "Lakini sijaiangalia. Nataka kufanya kazi nzuri. ... Bado inakaribia miaka minne."

Wabunge wengi wamepuuza maoni ya Trump kama tishio kubwa.

Kubadilisha Katiba kutahitaji idhini kutoka kwa theluthi mbili ya walio wengi katika mabunge yote mawili ya Congress, na vile vile kutoka kwa robo tatu ya majimbo, ambayo kwa hakika hayana nafasi ya kutokea.