Afisa wa polisi, Uganda

SIKU moja baada ya tukio la kustaajabisha lililotokea nje ya majengo ya bunge la Uganda ambapo mwanamume wa umri wa makamo alijichoma moto, idara ya polisi imevunja kimya kuhusu tukio hilo.

February 26, video zilisambazwa zikimuonyesha mwanamume aliyetambuliwa kwa jina Benjamin Agaba mmoja akijimwagia petroli na kisha kujiwasha moto nje ya majengo ya bunge ambapo kwa bahati nzuri walinzi wa bunge walimuokoa.

ASP Luke Owoyesigyire, naibu msemaji wa Polisi wa Metropolitan ya Kampala, alisema watu walioshuhudia walimwona Agaba kwenye Barabara ya Bunge akiwa na chupa iliyokuwa na kimiminika kinachoshukiwa kuwa petroli.

"Aliifungua, akajimiminia, kisha akapiga kiberiti ili kujichoma," Owoyesigyire alisema katika taarifa ya sauti.

"Walinzi bungeni walimkimbilia na kummwagia maji."

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Polisi walisema Agaba alipelekwa katika Hospitali ya Mulago, ambako anapokea matibabu.

×

"Uchunguzi unaendelea kubaini ni nini kilimpeleka kwenye hili, na tutatoa sasisho," polisi walisema.

Ripoti zinaonyesha kuwa Agaba alishutumu chama tawala cha National Resistance Movement (NRM) kwa kumpuuza.

Alidai NRM ilimtelekeza baada ya wafuasi wa upinzani wa National Unity Platform (NUP) kudaiwa kuharibu mali yake.

Pia alidai kuwa babake aliachwa bila makao kutokana na misimamo yao ya kisiasa. Agaba alisema alikuwa ametafuta usaidizi kutoka kwa ofisi za NRM kwa zaidi ya mwaka mmoja lakini hakupata usaidizi.

Taifa la Uganda linapitia kipindi cha mpito ambapo asilimia kubwa ya vijana wanaonekana kutoridhika na jinsi serikali ya rais Museveni inavyoendesha nchi hiyo jirani.Museveni amekuwa uongozini kwa zaidi ya miaka 30.