ALIYEKUWA naibu wa rais,
Rigathi Gachagua amedai kwamba eneo pana la Mlima Kenya sasa alina deni la mtu
yeyote zaidi ya kinara wa chama cha Wiper, Kalonzo Musyoka.
Akizungumza katika hafla moja ya mazishi kaunti ya Makueni, Gachagua alisema kwamba watu kutoka upande wa Mlima Kenya kazi yao ni ya kulipa madeni ya kisiasa.
Kiongozi uyo alibainisha kwamba kufikia sasa, wamemaliza kulipa deni la rais William Ruto kwa ujumla na sasa deni lililosalia ni la Kalonzo Musyoka.
“Sisi tulisahau kulipa Kalonzo deni lake, liko! Sisi ni watu wa kulipa madeni. Tulikuwa na deni la Ruto tumemaliza, sisi hatuna deni lake sasa. Tulikuwa tunataka kumlipa kwa awamu mbili lakini baada ya kumlipa awamu ya kwanza ameleta madharau tumesema hilo deni limekwisha,” Gachagua alisema.
“Sisi hatyuna deni lake, tuko huru sasa. Madeni ambayo tunayo ni kidogo kidogo ndio tunataka tulipe ndio tukae bila deni. Tumebaki tu na Kalonzo na nyinyi,” Gachagua alisisitiza.
Tamko hilo liliashiria kwamba huenda Kalonzo akaungana na Gachagua na viongozi wengine katika kuanzisha mrengo wa kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu wa 2027.
Gachagua alithibitisha kwamba kuna mazungumzo ambayo yanaendelea baina yake na viongozi wengine akiwemo Kalonzo Musyoka.
Alisema kwamba Kalonzo alionyesha urafiki wa kweli kusimama naye wakati wa mchakato wa kubanduliwa kwake ofisini.
“Tunaongea na Kalonzo, mimi na viongozi wengine kina Eugene Wamalwa na wengine na tutapanga vizuri. Tunafanya mazungumzo kama Wakenya tukitafuta njia vile tutajipanga vizuri kwa sababu ya uchumi wa Kenya yetu na tumalize mambo ya uongo katika hii Kenya. Tunataka hii Kenya isonge mbele,” aliongeza Gachagua.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!