SERIKALI kupitia wizara
ya leba imetangazia Wakenya wenye ujuzi katika kuendesha bodaboda kuhusu
kupatikana kwa ajira 600 katika jiji la Dubai, kwenye taifa la Miliki za
Kiarabu.
Waziri wa Leba Alfred Mutua alichapisha tangazo hilo kupitia ukurasa wake wa X, akiwataarifu Wakenya wenye ujuzi wa kuendesha bodaboda kutuma barua zao za maombi ya kazi.
Waziri Mutua alisema kwamba mshahara utakuwa shilingi 104,000 ambazo hazitoshwi ushuru.
Mutua alisema kwamba maafisa kutoka UAE watakuwa nchini Kenya wiki ijayo kutafuta waendesha bodaboda hao kwa ajili ya kazi hiyo ambayo itakuwa ni ya kupeleka na kurudisha mizigo na malipo yatakuwa yanahesabika baada ya kila mzunguko mmoja wa safari.
“Maafisa kutoka kampuni ya Umoja wa Falme za Kiarabu watakuwa nchini Kenya wiki ijayo kuwahoji na kuwaajiri waendesha pikipiki. Waendeshaji watapata dirham 7.5 kwa kila safari ya kusafirisha mizigo.”
“Wastani wa chini wa kila siku ni safari 15, kutafsiri hadi dirham 112.5 kwa siku. Kwa siku 26 za kazi kwa mwezi, hii ni jumla ya dirham 2,925 (takriban shilingi 104,000 za Kenya, bila kodi).”
“Wanunuzi walio na mpango wa kwanza wanaweza kusafirisha bidhaa zaidi ya 30 kwa siku, na kuongeza mapato yao,” Waziri Mutua alifafanua.
Hata hivyo, waziri Mutua alieleza kwamba yeyote atakayepata kazi hiyo atahitajika kugharamia ada mbalimbali zikiwemo usafiri, vipimo vya afya miongoni mwa ada zingine zitakazofika jumla ya shilingi 167,900 pesa za Kenya.
Lakini pia alifichua kuwa mpenyo wa yeyote atakayefaulu katika usaili lakini akakosa namna ya kupata pesa hizo, akisema benki ziko tayari kuwapa mkopo ambao watarejesha baada ya kuanza kazi Dubai.
“Benki zimeunganishwa ili kutoa mikopo ili kulipia gharama hizi, kuruhusu wafanyakazi kurejesha pindi wanapoanza kufanya kazi Dubai. Ada ya matibabu hulipwa kwanza, na gharama zilizobaki zinaweza kutatuliwa baada ya kupitisha matibabu. Hii inahakikisha hakuna hasara zisizo za lazima,” Mutua alifafanua kwa kina.
Usaili utafanyika Desemba 9-11 jijini Nairobi katika chuo cha kiufundi cha Kamkunji huku Malindi katika kaunti ya Kilifi usaili ukifanyika Desemba 13-14.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!