BENKI ya Uganda imetumbukia katika kashfa mpya baada ya wadukuzi kujipatia shilingi bilioni 2.2 (takriban dola milioni 17 za Kimarekani) kutoka kwa mifumo ya benki hiyo, jarida la The Citizen limeripoti.

Tukio hilo la udukuzi, ambalo linaaminika kutokea hivi karibuni, limezua maswali mazito kuhusu hatua za kiusalama zinazochukuliwa katika benki kuu.

"Ni kweli, Rais Museveni alimwagiza Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kuchunguza suala hilo," chanzo kilicho karibu na suala hilo kiliiambia CNN.

"Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali atabaini kiasi cha fedha kilichopotea katika udukuzi huo na kisha polisi watafuatilia pale ambapo kuna dhima ya uhalifu."

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Benki ya Uganda bado haijatoa maoni yoyote kuhusu wizi huo, lakini duru zinasema uchunguzi uko katika hali ya juu, huku maafisa wa ngazi za juu wakihojiwa na polisi na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Benki kuu imekabiliwa na kashfa katika miaka ya hivi karibuni, ikiwa ni pamoja na wizi wa noti za zamani na maafisa wake.



Katika kesi mashuhuri, Charles Kasede Ochieng, aliyekuwa Mkuu wa Uhakiki, alihukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela kwa kutumia vibaya nafasi yake kuiba noti kuukuu zilizokusudiwa kuharibiwa.

Kashfa ya hivi punde imeibua wasiwasi kuhusu uwezo wa benki hiyo kulinda mifumo yake na athari zinazoweza kujitokeza kwa uchumi wa nchi.

Benki ya Uganda imekuwa bila gavana tangu kifo cha Emmanuel Mutebile Januari 2022.

Hii si mara ya kwanza kwa tukio la udukuzi kufanyika katika mifumo ya Benki kuu ya Uganda.

Mnamo Agosti 2020, ripoti ziliibuka kwamba wadukuzi walifanya jaribio la kutaka kuiba dola milioni 24 baada ya kudukua mitambo ya benki hiyo.


Kwa mujibu wa ripoti wakati huo, akaunti ambazo zililengwa ni zile za idara zenye mgao mkubwa wa bajeti kama wizara ya ulinzi, kawi, ujenzi wa miundombinu na kilimo.


Hata hivyo, baadhi ya pesa ambazo zilikuwa tayari zimehasmishiwa kwa akaunti zilizokuwa Hong Kong na UAE zilifaulu kurudishwa.


Tayari, rais Museveni ametoa agizo la kufanyika kwa uchunguzi dhidi ya udukuzi huo ambao umeonekana kuwa donda sugu kwa usalama wa mifumo ya benki ya Uganda.