Mtoto wa marehemu mwimbaji wa Kikuyu Benga John De’Mathew na mkewe wa pili Carolyne Waithera, Tyrese Thiiru, alimaliza masomo yake ya shule ya upili mnamo Ijumaa, na familia yake haikuweza kuficha furaha yao.
Tyrese, ambaye ni mtoto wa kwanza wa marehemu De’Mathew na Waithera, alikuwa miongoni mwa wanafunzi zaidi ya 900,000 waliofanya mtihani wa KCSE 2024. Alikuwa mwanafunzi katika Shule ya Upili ya Thika maarufu katika Kaunti ya Kiambu.
Kama tu wanafunzi wengine wengi waliomaliza masomo yao ya shule ya upili wiki iliyopita, Tyrese alichukuliwa kutoka shuleni na familia yake. Njia ambayo alichukuliwa kutoka shuleni hata hivyo ilikuwa maalum kwani alipata mapokezi ya kifalme kutoka kwa familia.
“Jamani, Mtoto wangu amemaliza shule. Mimi ni mwanamke mwenye kujivunia leo. Nimefurahiya sana. Ninamwendea mwanangu katika Shule ya Upili ya Thika, Mtoto wangu amemaliza shule. Bwana wangu, nitamwambia nini Mungu? Nitaambia Mungu nini sasa aki? Kumshukuru hawezi tosha,” Bi Waithera aliyekuwa na furaha kupita kiasi alisema alipokuwa akielekea kumchukua mwanawe shuleni.
Mhitimu huyo mpya wa kidato cha nne alichukuliwa kutoka shuleni na Limousine nyeupe aina ya BMW yenye mabango yaliyoandikwa "Hongera, Tyrese Thiiru."
Aidha, zulia jekundu liliwekwa chini kwa ajili yake, na walinzi waliojengeka misuli vyema walimsindikiza huku akipokelewa na familia.
“Umeona alichokifanya Bwana? Hili ndilo nililoomba,” Bi Waithera alisema baada ya kumchukua mwanawe.
Namna Tyrese alivyochukuliwa shuleni ilipokelewa kwa hisia mseto, huku baadhi ya wanamtandao wakimpongeza, wengine wakitoa maoni yao kuhusu kitendo hicho cha bei ghali, na wengine hata wakimkosoa mama huyo.
“Aty atapata D-, ata akipata X,Y,Z mtoto ni wangu,” alisema.
Aliongeza, “Mliskia ata akipata W ama Q mtoto ni nani? Nani analipa ada? Hongera sana Edward wangu.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!