Kane

Harry Kane ameandikisha historia kwa kufunga jumla ya mabao 50 kwenye Ligi Kuu ya Ujerumani maarufu Bundesliga.

Kane amefikia mabao hayo kwa kasi ambayo haijawahi kushuhudiwa alipofunga hat-trick iliyoipatia Bayern Munich ushindi wa 3-0 dhidi ya Augsburg.

Nahodha huyo wa England alihitaji kufunga mabao matatu tu kuandikisha historia hiyo.

Kane amefunga mabao 50 katika mechi 43 za Bundesliga kumaanisha kuwa amevunja rekodi ya Erling Haaland ya kufunga mabao 50 katika mechi 50 alipokuwa akichezea klabu ya Borussia Dortmund, kabla mchezaji huyo wa Norway kujiunga na Manchester City.

Ushindi huo uliwafanya Bayern kuwa pointi nane mbele ya Leipzig kileleni mwa ligi kabla ya mechi za wikendi.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Wababe hao wa Ujerumani hamepata ushindi mara tisa na kutoka sare mara mbili katika mechi 11 walizocheza.