
Mbunge wa Mumias ya Mashariki Peter Salasya
ametangaza rasmi vita yake ya kuhakikisha anatokomeza ushawishi wa kinara wa
chama cha ODM katika eneo la Magharibi mwa Kenya.
Kupitia video aliyorekodi, Salasya alisema kwamba
tayari wameanza kutoa elimu ya kiraia kwa watu kuwaeleza jinsi watakavyoweza
kusonga mbele kisiasa bila Raila Odinga katika eneo pana la Magharibi.
“Tumeshaanza
kufanya zoezi la kutoa elimu ya kiraia, tukiwaambia watu wetu kutoka Magharibi mwa
Kenya Raila Odinga ni nani,” Salasya alifichua.
Mbunge huyo kijana alidai kwamba Odinga tayari
ameitisha kikao na wanachama wa Odinga katika kile alisema ni kuanza kuwatishia
dhidi ya kutonena kwa sauti moja ya muongozo wa chama.
“Na
baada ya kusikia hivyo naambiwa ameita mkutano na wananchama akiwatishia kwa
kutumia kamati za bunge. Ningependa kuwaambia watu kutoka Magharibi, wale
waheshimiwa wanaoenda kumuona, ni kwamba tu kama hawawezi onyesha mshikamano
watatolewa kwenye kamati za bunge,” Salasya alidai.
Mbunge huyo wa chama cha DAP-K alisisitiza kwamba
msimamo wa watu kutoka Magharibi hautakuwa wa kupangwa bali watashawishika na
ajenda na rekodi ya maendeleo.
Akionekana kuwalenga wale wanaomkosoa, Salasya
alisema kuwa yeye ni Gen Z ambaye haogopi kitu chochote kando na kuoa tu.
“Mnanitishia
mkinitusi mmesahau kwamba mimi ni Gen Z, kizazi changu sisi hatuogopi kitu
chochote, tunachoogopa ni kuoa peke yake. Sasa mimi nataka niwaambie ya kwamba
waite lakini sisi tunaanzisha mchakato wa kuenda kwa ground,”
Salasya alisema.
Mbunge huyo alimtuhumu Odinga kwa kile alisema ni
kuitetea kampuni ya Adani ambayo inalenga kuchukua kandarasi ya kuendesha
uwanja wa ndege wa JKIA kwa miongo mitatu.
Salasya pia alidai kwamba Odinga analenga kusukuma
kuondolewa kwa hela za ustawishaji wa maeneo bunge, CDF na kupelekwa chini ya
usimamizi wa magavana.
“Eti
unataka CDF na KeRRA itolewe kwa kiwango cha maeneo bunge na ipelekwe chini ya
usimamizi wa magavana, eti halafu nikuunge mkono, mimi ni mwendawazimu?”
Salasya aliuliza.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!