MWANAMKE mmoja aliyekuwa mjamzito amefariki baada ya kutokwa damu kupita kiasi wakati wa jaribio la kumkeketa lililoenda mvange katika kaunti ya Elgeyo Marakwet.

Mwanamke huyo aliripotiwa kufa mikononi mwa wanawake wenza ambao walijukumiwa na  shughuli ya kumfanyia kitendo hichi kilichopitwa na wakati.

Wake wenza hao walifanyiwa ukeketaji ulioharamishwa katika eneo la Kocholwo, kaunti ndogo ya Keiyo Kusini alfajiri ya Jumanne lakini iligeuka msiba baada ya mama mdogo kufariki kutokana na kuvuja damu nyingi.

Mwanamke mkubwa alikimbizwa katika hospitali ya karibu. Kulingana na mamlaka, wake wenzi hao wanaweza kuwa walilazimishwa na waume zao kumfanyia unyama huo.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Siku ya Jumatano, polisi walikuwa bado wanamfuatilia mwanamume huyo mwenye wake wengi ambaye inasemekana alitoroka baada ya mke mdogo kufariki.

Naibu Kamishna wa Kaunti ya Keiyo Kusini, Diana Wekesa jana aliambia vyombo vya habari kwamba uchunguzi wa awali unaonyesha mumewe alipanga tohara hiyo.

Bi Wekesa alisema tohara ilifanywa kisiri nyumbani kwa mwanamume huyo. Mke wa marehemu, kulingana na maafisa wa polisi wanaochunguza kisa hicho, alikuwa na umri wa miaka 26 huku mke mkubwa akiwa na umri wa miaka 40.

Bi Wekesa alisema polisi walikuwa wakimhoji mwanamke mwenye umri wa miaka 70 anayeshukiwa kutekeleza kitendo hicho.

“Tahadhari ilitolewa Jumanne mchana kwamba mwanamke ambaye alikuwa amekeketwa alikuwa ametokwa na damu nyingi. Chifu msaidizi wa eneo hilo alikimbia hadi eneo la tukio ambako ndiko nyumbani kwa wake wenzake na kugundua kuwa mke mdogo alikuwa tayari amefariki,” alisema jana.

Alisema ziara ya mamlaka katika nyumba ambayo tohara ilifanywa iliripoti kuwa eneo lilikuwa limejaa damu.