Wasanii wakubwa wa nyimbo za injili wa Afrika Mashariki Christina Shusho wa Tanzania na Israel Mbonyi wa Rwanda watazuru Kenya mwishoni mwa mwezi ujao.
Waimbaji hao wawili wa nyimbo za injili wanaofurahia ufuasi mkubwa nchini Kenya wamethibitisha kwamba wataungana na Wakenya kuvuka mwaka hadi 2025 mnamo usiku wa Desemba 31.
Huku akithibitisha tamasha lake la Kenya, Bi Christina Shusho alidokeza kuwa kutakuwa na wasanii kadhaa wa kuvutia ambao watatumbuiza naye mwishoni mwa mwaka.
“Ndugu zangu kuna sehemu moja tu ya kuvuka. Tuna mpangilio wa kuvutia," Christina Shusho alitangaza.
Mbonyi kwa upande wake pia alithibitisha kuwa atazuru Kenya kwa tamasha la kuvukisha mwaka.
"Hujambo Kenya, 31 Disemba #CrossOver," Israel Mbonyi alisema.
Wasanii hao wawili wa injili wanathaminiwa sana na kushabikiwa sana nchini Kenya. Wamewahi kufanya ziara tena nchini katika siku za nyuma.
Christina
Shusho alikuwa nchini mwishoni mwa mwaka jana na alitumbuiza usiku wa Desemba
31, 2023.
Mbonyi alikuwa nchini mwezi Agosti ambapo alifanya shoo kubwa iliyovuta mashabiki wengi.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!