caption
Watu 14 waliuawa na wengine 34 kujeruhiwa baada ya radi kupiga kanisa katika wilaya ya kaskazini mwa Uganda ya Lamwo Jumamosi, polisi walisema.

Kanisa hilo liko katika kambi ya wakimbizi ya Palabek.

Msemaji wa polisi wa Uganda Kituuma Rusoke alisema tukio hilo lilitokea mwendo wa saa 5:30 asubuhi. wakati waathiriwa walikuwa wamekusanyika kwa ibada ya maombi.

"Tukio hilo lilitokea wakati wa ibada ya maombi katika kanisa la Zone 8, Block 2. katika kambi ya makazi ya Palabek," Rusoke alisema katika chapisho la Jumapili kwenye X.

"Waathiriwa, ambao bado hawajatambuliwa, walikuwa wamekusanyika kwa ajili ya maombi wakati mvua ilipoanza.

Matukio hayo ya kupigwa na radi ni ya kawaida nchini humo, mnamo Juni, tukio kama hilo lilitokea katika shule moja katika Wilaya ya Nebbi kaskazini mwa Uganda na kusababisha wanafunzi 77 kujeruhiwa

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans