Uchafuzi wa hewa unasalia kuwa tishio kubwa la kimazingira kwa afya ya umma nchini huku raia wakiwa katika hatari ya kupata viwango vya uchafuzi mara nne zaidi ya mwongozo uliopendekezwa na Shirika la Afya Duniani (WHO). Taarifa ya Uchafuzi ya Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) inaonyesha kwamba Wakenya wanakabiliwa na wastani wa mikrogramu 20.3 kwa kila mita ya ujazo ya chembe chembe ndogo kila mwaka. Imeorodhesha Kenya miongoni mwa nchi zinazokabiliwa na uchafuzi wa hewa.