Rais wa Chama cha mawakili LSK Charles Kanjama anasisitiza kwamba majaji wanapaswa kupitishwa kwa viwango sawa vya uwajibikaji kama maafisa wengine wa umma, akisisitiza kwamba mahakama lazima iruhusu vyombo vya kikatiba kutekeleza jukumu lao. Kanjama aliwashutumu baadhi ya majaji kwa kuzuia uchunguzi unaofanywa na Tume ya Huduma za Mahakama na Tume ya EACC kupitia amri za mahakama. Alisema hatua hiyo inalenga kukuza uwazi, ufanisi na mfumo wa haki usioingiliwa.

CHARLES KANJAMA – ACCOUNTABILITY