Rais wa China Xi Jinping alikutana na Rais wa Marekani Donald Trump mjini Busan, Korea Kusini, Oktoba 30, 2025. (Xinhua/Huang Jingwen)
Rais wa China Xi Jinping alisema hapa Alhamisi kuwa China na Marekani zinapaswa kufanya kazi pamoja kutimiza mambo makubwa na ya vitendo zaidi kwa manufaa ya nchi zao mbili na dunia nzima.
Alitoa kauli hiyo wakati wa mkutano na mwenzake wa Marekani, Donald Trump, baada ya kuwasili Busan kwa ajili ya Mkutano wa 32 wa Viongozi wa Kiuchumi wa APEC mjini Gyeongju, na ziara ya kiserikali nchini Korea Kusini.
Xi alibainisha kuwa Rais Trump ana shauku kubwa ya kutatua masuala mbalimbali yenye mvutano wa kikanda, na kwamba China pia imekuwa ikiendeleza mazungumzo ya amani ili kutatua masuala mbalimbali ya mvutano.
Akisema kuwa dunia ya leo inakabiliwa na matatizo mengi magumu, Xi alisema China na Marekani zinaweza kwa pamoja kubeba wajibu wao kama nchi kubwa.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!