
MKE mmoja amezua mjadala mtandaoni baada ya kufichua kwamba alimlipisha mumewe zaidi ya dola milioni 3.5 na kuomba gari la kifahari kama zawadi ya kujifungua mtoto wao wa pili.
Alifanya ufichuzi huo katika chapisho lililoshirikiwa kwenye X (zamani Twitter), akivutia maoni tofauti kwenye mitandao ya kijamii.
Katika chapisho hilo, mwanamke huyo alielezea gharama za kifahari ambazo mumewe alitarajiwa kulipa - kutoka kwa mitindo ya kifahari hadi ukarabati wa nyumba - yote yakilenga kumpa binti yao mchanga maisha mazuri na ya starehe.
Alieleza kwamba baada ya kujifungua, alimshrutisha mumewe kumpa gari la kifahari aina ya G-Wagon Brabus la rangi ya pink pamoja na pesa taslimu Sh453,465 kwa matumizi mbalimbali.
Kauli yake: "Mwanzo wa kwanza, G-Wagon ya waridi iliyopewa nambari ya usajili ya jina langu kama zawadi yangu kwa kumpa mtoto wa kike, $2 milioni kwenye nyumba mpya, $1 milioni kwa ukarabati na mambo ya ndani, $100,000 kwenye mifuko minane ya Dior, $80,000 kwenye mkusanyiko mpya wa Van Cleef, na $10,000 kwa masaji ya kila siku baada ya kujifungua."
Aliendelea kuorodhesha gharama kadhaa zaidi, ambazo zote ziliripotiwa kufadhiliwa na mumewe baada ya kuzaliwa kwa mtoto wao wa pili.
Chapisho hilo lilisambaa kwa kasi, na hivyo kuzua hisia nyingi huku watumiaji wakifurika sehemu ya maoni ili kushiriki maoni yao kuhusu ishara hiyo ya upendo ya kupindukia.
Tazama video hiyo hapa chini;
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!