Ruben Amorim

RUBEN Amorim amesema Manchester United wako "katika haraka" kuimarika na kutinga kileleni mwa Premier League.


United wamo katika nafasi ya 13, kwa sasa wakiachwa kwa pointi 35 na vinara wa ligi Liverpool, huku kukiwa na mechi 7 pekee kumalizika.


Lakini Amorim alisema anatumai United itaonyesha maboresho yanayoonekana kufikia msimu ujao.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans


Mkufunzi wa Manchester United Ruben Amorim alisema klabu hiyo iko "haraka" kuwania mataji ya Premier League.


Akizungumza kabla ya mechi ya Jumapili ya Manchester derby dhidi ya mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Uingereza Manchester City, Amorim alisisitiza kuwa anatumai kuona timu yake ikiimarika ifikapo msimu ujao.


"Ninaelewa, lakini mimi sio limbukeni. Sitaki kufikiria tunahitaji miaka mingi ili tuwe na ushindani. Siwezi kufikiria hivyo, siwezi kusimamia hilo, haliko ndani yangu. Ndiyo maana ninajipa shinikizo.


"Najua hatutakuwa wapinzani wakubwa katika mwaka ujao au miaka miwili ijayo. Tunabadilisha mambo mengi ndani ya klabu na tunajua itachukua muda mwingi, lakini sitasema nahitaji miaka mingi.


“Mwaka ujao ndio lengo letu, sisemi tutatwaa ubingwa mwakani, sina kichaa.”


"Mimi nasema sitaki mazungumzo haya ambayo tunahitaji miaka mingi na tuyaweke utulivu - hapana, tuko katika harakati za haraka. Tunateseka sana kwa mwaka ujao kuwa bora zaidi.


"Sitaki kuwa mtu ambaye ameketi hapa akisema tunahitaji muda mwingi. Sitakuwa kocha huyo."


Amorim alikiri kwamba vilabu vilivyo mbele yake vitakuwa bora zaidi msimu ujao na kwamba angependa kuleta "mchezaji mmoja au wawili wakubwa" ili kuimarisha kikosi cha United.


“Timu zote tayari zipo sehemu ambayo tunahitaji sana kuzinasa na zitaimarika tena msimu ujao, nataka tuzingatie nguvu zetu kisha tuitumie klabu yetu kujaribu kuleta mchezaji mmoja au wawili wakubwa,” alisema Amorim.


"Siwezi kuvumilia kusema kwa miaka mitatu, bado tunajaribu kitu. Kwangu, tutaanza msimu ujao. Tunahitaji kuwa bora zaidi kwa sababu hii ni klabu kubwa na ninataka kuweka shinikizo hilo kwangu na kila mtu hapa."