
Mawaziri wa mambo ya nje wa kundi la mataifa ya G7, ikiwa ni pamoja na Marekani, Uingereza na mataifa mengine yenye nguvu barani Ulaya, wanakutana kwa siku yao ya mwisho ya mazungumzo nchini Canada, kufuatia mgawanyiko kuhusu kauli ya pamoja kuhusu Urusi na vita nchini Ukraine.
Mwenyeji Canada, waziri wa mambo ya nje Melanie Joly, aliketi karibu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio na kusema G7 lazima iunge mkono Ukraine dhidi ya kile alichokiita uchokozi wa Urusi.
Lakini Marekani inakataa shutuma hizo za umma dhidi ya Moscow, ikisema lugha hiyo ni ya kuchukiza wakati Rais Donald Trump anajaribu kuzishawishi pande hizo mbili kukubaliana kusitisha mapigano mara moja.
Taarifa za awali za pamoja za G7 zimejumuisha shutuma kwa Urusi, Kuonyesha mgawanyiko mkubwa kati ya Ulaya na utawala wa Trump juu ya wapi jukumu la vita linapaswa kuhusishwa.
Mataifa ya Ulaya yanaunga mkono wito wa Trump wa kusitisha mapigano, lakini bado wanaamini Moscow inapaswa kuitwa wazi kwa uvamizi wake kamili wa Ukraine.
Siku tatu baada ya Ukraine kukubali makubaliano ya kusitisha mapigano ya siku 30, Rais wa Urusi Vladimir Putin alijibu pendekezo la Marekani - lakini haikuwa ndiyo au hapana.
Putin alisema, anakubaliana na wazo hilo, lakini akaweka masharti magumu na kusema "maswali" yamebaki kuhusu usitishaji mapigano.
Alisema usitishaji wa mapigano unapaswa kuondoa sababu za mgogoro huu. Akiongeza kuwa nchi hiyo ya Urusi inahitaji kufanya mazungumzo na Marekani. "Labda nitakuwa na mazungumzo ya simu na Donald Trump," alisema.
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky naye ameelezea majibu ya Putin kama "ya kipuuzi" na kutoa wito wa vikwazo zaidi dhidi ya Urusi. Putin hakusema moja kwa moja, alisema katika hotuba yake ya video ya usiku.
Maafisa wa Urusi wamesema Putin alitarajiwa kukutana na mjumbe maalum wa Marekani Steve Witkoff, ambaye alikuwa amesafiri kwenda Moscow mapema siku hiyo - lakini haijabainika iwapo mkutano huo ulifanyika.
Siku ya Ijumaa, vyombo vya habari vya serikali ya Urusi vilinukuu tovuti ya ufuatiliaji wa safari za ndege ya Flightradar ikisema ndege inayoaminika kuwa imebeba Witkoff iliondoka Moscow.
Nchi zote za Urusi na Ukraine zimeripoti mashambulizi mapya ya ndege zisizokuwa na rubani. Ukraine imesema watu saba wakiwemo watoto wamejeruhiwa katika mji wa kaskazini mashariki wa Kharkiv. Urusi nayo iliripoti moto mkubwa katika kituo cha mafuta katika mji wa kusini wa Tuapse.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!