Mwanasoka wa Ufaransa Paul Pogba amehitimisha rasmi marufuku yake ya kutoshiriki kwenye kandanda ya miezi 18  baada ya kupatikana na hatia ya matumizi ya dawa za kusisimua misuli.

Kulingana hukumu iliyotolewa upande wake kifungo hicho kinakamilika kuanzia Machi 10, 2025, na kumpa nafasi nyingine ya kurejea uwanjani na kuhusika moja kwa moja kwenye soka ya kulipwa.

Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 31 alikua mchezaji huru kufuatia uamuzi wa Juventus kusitisha mkataba wake mnamo Novemba 2024.

Kusimamishwa kwake kulitokana na upimaji wa Pogba na kupatikana na virusi vya testosterone visivyo vya kawaida kufuatia mechi ya Serie A dhidi ya Udinese mnamo Agosti 20, 2023.

Awali alikabiliwa na marufuku ya miaka minne, adhabu hiyo ilipunguzwa hadi miezi 18 na Mahakama ya Usuluhishi wa Michezo (CAS) mnamo Oktoba 2024, na kumpa mchezaji nafasi ya kurudi kwenye mchezo mapema kuliko ilivyotarajiwa.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Baada ya kusimamishwa kwake, Pogba alibaki kujitolea kudumisha hali yake ya kimwili kupitia mazoezi ya kibinafsi.

Ripoti zinaeleza kuwa kiungo huyo mzoefu ana hamu ya kuanza upya kazi yake na ana hamu kubwa ya kuendelea na safari yake katika moja ya ligi tano bora barani Ulaya.

Hamu yake ya kurejea Ufaransa pia imeangaziwa, huku Olympique de Marseille ikiibuka kama mshindani mkubwa wa saini yake wakati wa dirisha lijalo la uhamisho wa majira ya kiangazi.

Licha ya kuwa nje ya mchezo kwa muda mrefu tangu Septemba 2023, Pogba amedhamiria kurejesha hali yake na kufanya kazi ili kupata nafasi katika timu ya taifa ya Ufaransa kabla ya Kombe la Dunia la FIFA la 2026.

Mchezaji huyo wa zamani wa Manchester united amepata mafanikio makubwa katika soka, ikiwa ni pamoja na mataji manne mfululizo ya Serie A na Juventus na jukumu muhimu katika ushindi wa Ufaransa wa Kombe la Dunia 2018.

Wakati akipitia awamu hii muhimu, wapenzi wa soka duniani kote wanafuatilia kwa karibu hatua yake inayofuata, wakitarajia athari zake uwanjani atakaporejea.

Maswali mengi kwa sasa miongoni mwa wapenzi wa soka ni  kwamba ataingia timu gani na katika ligii ipi kueneleza kipaji chake cha soka.